UTENZI:NAKULILIA MAGUFULI

POEM NO 16
POEM NO 16

 1.

Mwangaza umeshazima

Nchiyo inazizima

Vitu vyote mesimama

Tumebaki ka yatima.


2.

Flayova alijenga

Mishahara bila chenga

Wananchi walilonga

Shida zao kaziganga.


3.

Miji yote iling'aa

Kwa umeme kusambaa

Kila kona ya mtaa

Magufuli aliweka.

4.

Elimu bure shuleni

Wanafunzi kasomeni

Madawati darasani

Magufuli alipania.


5.

Bodaboda barabara

Zimejengwa kwa imara

Mutembee kwa busara

Magufuli alijenga.


6.

Ni kilio kwa hakika

Nchi imetikisika

Machozi yanatutoka

Magufuli kaondoka.

7

Imekuwa ni mapema

Kuondoka ulo mwema

Ulale mahali pema

Raisi wetu magufuli.

8.

Watumishi uliahidi

Neema kuzifaidi

Mapato yatapozidi

Hakika ulipania.

9.

Uchungu menilemea

Mbele sitoendelea

Machozi yamenijia

Magufuli nakulilia.


Itaendelea........

Utenzi umeandikwa na 

Mwl Godoni Y Bayalimo

Mnamo tar 21.03.2021 kufuatia kifo cha aliyekuwa raisi wa Tanzania kilichotokea tar 17.03.2021.



Comments

Amos Ngarama said…
Utenzi meusoma
Kwa umahili hakika
Menivutia sana
Kwayo mawaidha
Pongezi pokea
Wala sipuuzie.
������������.

Dogo uko vizuri sana
Godoni said…
Sawa kaka.Tunaendelea kujifunza.

Popular posts from this blog

UNTOUCH YOUR FATHER'S BEARDS by mwl Godoni Yohana

Mu wapi malenga? by Godoni Yohana.